MTAFITI

Wednesday, April 26, 2006

motro uliaka!

Uwongo si kazikutugwa na hata mtu kuandika lakini leo nimekubali....ni muda mrefu sijawajulia hali ndugu ,jamaa, marafiki,wanafikina ,waungwana na hata maadui,Hawa wote huwa tunakutana katika haya makazi yasiyokuwa na mipaka.
Ndesanjo naona moto wa blog unawaka moto wa kasi mithili ya nyumba ya nyasi(Ngaamba fulu suti mmba sa kulya mndeni oh manya mmba sa haa uenini sejengwa kwa mfiri saba na iingua kwa dakika tanu.UUh ngaamba ngiliisha se iblogu..ngebaki nyuma foo laiki ikoti...
karibuni wooose fuu mmba!

Friday, February 03, 2006

Je unajua hili??

Nipo bado ijapokuwa kuna ambao wamesema ameingia mitini huyu.Nipo katika harakati za kujifunza masuala ya kutunza afya pasipo kutumia dawa.Dawa zilizitengenezwa kwa kutumia kemikali.
Nimekuwa na furaha mno na kupenda kuwashirikisha hilli leo.Tafiti zimefanya na kugundua kuwa..
1.Kucheka ni dawa kubwa mno kwa binadamu..na kusema kuwa watoto wanauwezo wa kucheka mara 10,000 kwa juma..na watu wazima mara 5.Sasa kucheka kunasaidia kinga ya mwili kuimarika..Haya jamani hebu chekeni kidogo.
2.Tabasamu..kutabasamu kunasaidia pia kinga ya mwili..kutokana na mishipa mingi kuwa katika paji la uso ambayo huamsha sehemu zingine za mwili na kuziweka katika mwelekeo sahihi.
3.Jenga tabia ya kukumbatia watu..(hugs)Hii inasaidia mwili kukua na kujisaidiia wenyewe pasipo msaada wa kemikali.Tafiti zilibaini kuwa watoto wadogo wanaokuwa walifanyiwa majaribio.Walipewa chakula na kila kitu wanacho hitaji kwa mwili..lakini hawakukumbatiwa au kupewa busu.Wale watoto hawakukua.Sasa Jenga tabia hiyo..Jiulize leo nimekumbatia watu wangapi?Inabidi ujifunze.
4.Namalizia kwa kusema kuwa mtu wa kupenda kusema asante.Ni neno dogo lakini liseme kila wakati unapoaamka..unapokula ..Hilo neno ni zito na lina umuhimu wake na utajisikia vizuri ukilisema kwako mwenyewe na kuwaambia wengine.
Asante!

Friday, January 06, 2006

Heri ya mwaka mpya.

Nglaafo ngera ya sisi,ngilemaa mwaka..Heri ya mwaka huu uhiyaa kwa moni wasomii wakwa.
Nimerudi mwaka mpya hivi nikiwa na mambo mengi ..sitaki kutumia usemi aliotumia mgombea uraisi wa wadanganyika..nitake kuwakoga na nyie wengine.Haya Basi mwaka umeanza na vijimambo vyake..
Nipende tu kuwashirikisha wanaglobu wenzangu huu mwaka nimepania na ninaweka mtazamo makini nataka kusoma vitabu.Macha alishanieleza ni kwa kiasi gani ukisoma unapata mwanga..sasa mimi mwenzenu nia yangu kubwa ni kuhangaika na vitabu.
Hebu jiulize ni vitabu gani hivi huyu mtafiti anataka kusoma??????
Nimeanza kusoma vitabu vya tiba za asili,tiba za matunda,majani ,maji,mizizi iliradi kisiwe kinahusisha mashine na kuongezwa kemikali.Hiyo ndio hoja nayoanza nayo mwaka huu.Kwa hiyo kaaeni mkao wa kula,angalau kila siku naweza kuwatumia dawa kidogo mkasoma na kutumia.
Nilishawadokeza ya mkojo kidogo,sasa nitaileta kwa undani..na kwa taarifa yenu kama kuna mtu anata kujaribu nasema fanya utaaona matokeo yake.Hapa leo sipo kutoa shuhuda lakini nasema mwaka huu najali afya yangu na wanablog wenzangu nasema afya yako ni muhimu.
Haya kwa taarifa ya juu juu..anza kula vitu ambavyo unaweza KUTAAMKA KWA ULIMI WAKO ,UKALA.Hicho unaweza kutumia..kama huwezi basi ujue si kizuri kwa afya yako.
Mwaka mpya huu jamani mlio na watoto muache kuwalishe zile wnazoita fomula..maana ni mengi yaliyopo huko,watumiaji wa manukato hasa ya kwenye makwapa(Deodorants)Muache hasa wanawake inasemekana inachangia kwa kiasi kikubwa saratani ya ziwa.Mpo hapo?Watumiaji wa majiko ya kupasha moto chakula(microwave) macho haya tunayapoteza.
Uhondo wa ngoma uingie ucheze na shughuli ipate mkunga!

Friday, December 23, 2005

NINGEKUWA NA MABAWA....

Ningekuwa na mabawa ningeruka upesii..Nyumbani mbali..ni nani asiyepata ugonjwa wa kukumbuka nyumbani hasa inapofika wakati wa sikukuu???????Ninatembea barabarani,ninatazama huku na kule nikijaribu kubadili mazingira kwa akili na macho yangu,nafunga macho, nafungua ni pale pale ambapo nimekuwepo,hakuna jipya zaidi ya mapambo na harakati za sikuuu..
Heka heka za manunuzi ya mwisho mwisho wa sikukuuu ya Noeli ndio hivyo yanatia tamati muda si mrefu.Ni maduka makubwa machache ambayo yatakuwa wazi.Watu wanasafiri,barabara ,viwanja vya ndege vimejaa watu wako mbioni kuungana na familia na mrafiki kwa ajili ya sikuuu.Hizi ni harakati ambazo zinaendelea kwa hali ya juu hapa nilipo.Wafanyao kazi,wengi wao wanasiku kadhaa za mapumziko.Ni shamra shamra zinaendelea hapa Nyumbani kwa Joji Kichaka.
Ninakumbuka nyumbani,ninakumbuka Tanzania,ninakumbuka Dar-es salaam,Ninakumbuka Rombo.Nauli za kuelekea Kilimanjaro zimekuwa "iyo la njofuu"Kila mtu anataka kupanda basi la Meridia kwenda Rombo.Watu wamekuwa wengi nauli haishikii..lakini hakuna anayekubali kusherehekea noeli darisalama.Maamuzi ya kukaa kwenye kigoda masaa nane yanawakumba wasafiri wa dakika za mwisho .Hiyo ndio hali halisi,kituo cha basi cha ubungo kimeshehena watu..ni majira ya saa tisa na nusu na kumi alfajiri mabasi yanaondoka.Yameanza kuwasha taa na honi zikipigwa kwa wingi.Ni mashamu shamu na manjonjo ya sikukuu tu hayo.Bila kusahau polisi wa usalama barabarani nao wanamengi ya kusema na madereva.
Ni foo shuruni kulwayaa mndeni,waiinu waliisha isherikia krismasi,mengele si meshiha,si isafii,umbe sa amii fo shii,mahorima.Kwentrwe maruwa,umbe silishinjwa,mburu,kisusio,umbeke kwentre kila mrii..ndisi na mshele umewa tayari kwa jumapili we kora pilau na shapati.Kwa fungua redioo waishua foo Kenya wakakaba Jim revees nyimbo saChirsmas.Foo makaniseni kwentrewe misa sa kiyoo,hashe hashe kona waliimba.Ngaamba kwentre chrismas mndeni laaya handu we manya kwetre skukuu.
HASHE HASHE KONA !!

Wednesday, December 14, 2005

Kumekucha.

Hivi siwezi kuaminini mwezi sasa umepita tangu niingie humu ndani ya nyumba yangu kusema lolote.Hivi ni mwaka huu umekuwa mfupi au nimekuwa na mambo mengi kIasi nasema kuwa muda ulikuwa mdogo.
kuna mwanablogu mmoja huwa anasema masaa 24 huwa haya mtoshi na sema tena sasa nimeamini nitaacha kutania ambao wanadai masaa 36.
Mchana wa leo umekuwa mtulivu kidogo kwangu baada ya kumaliza mitihani yangu ya muhula kama lisaa limoja lililopita.Nimerudi katika ulimwengu wa kutoa maoni yangu kwa kutumia mtandao.
Ulimwengu wa Blogu umekuwa na mafanikio bila kipingamizi na kuna mwamko wa pekee unaendelea katika jamii ya waafrika wazungumzao kiswahili.Na hao sio wengine ni wa Tanzania wenzangu ambao wamekuwa wakijiunga kila siku kukicha katika hii tekinolojia.Nasema tena karibuni watanzania wenzangu tuweke yanayotusibi hata kama hawasomi watayasikia kupita hapa ama pale.Hongera sana kwa wale ambao wamekuwa wakijiunga kwa wingi,naweza kusema mwaka 2005 umekuwa na changamoto ya pekee kwa wana globu.Hongera kwa watu ambao hawako nyuma kutupa viunganishi vya globu mpya mara zinapoingia..si Mwingine bali ni NDESANJO.http://jikombe.blogspot.com

Monday, November 14, 2005

Sema utakacho.

Mfiri n'ganyaa fo nyumaa nilikuwa natembelea blogu mbali mbali na kuangalia nini hasa kinaongelewa na nini hasa, nani anajisikia kuandika nini.
Nilifurahi sana na dhani nilitumia muda wa masaa mawili tu kusoma nini wanablogu kama mimi wanasema na kujifunza.
Siku kadhaa niliahidi nitaandika kuhusu televisheni.Laah leo nimepata zuri zaidi lipi hilo.
Nimeingia katika fani ya afya.Nilikuwa nasoma kuhusu mkojo na tiba zake.Ahh ni mengi nitaandika tena .Bado nasoma makala tofauti tofauti kupitia wandishi tofauti na kurasa tofauti za mtandao.

Monday, November 07, 2005

je huu ni ubaguzi??

Nina kazi ya darasani ya kuandika kuhusu jamii na utazamaji wa luninga.nimeshindwa kusema ama kuandika vizuri kutumia kiswahili hata kile kichaga.mada yenyewe inasema hivi"Ethinicity&race has been a long time issue on television."
Hapa nitakuwa nazungumziua jinsi televisheni zimekuwa zikionjesha aina fulani za jamii na yanayowazunguka.. katika vipindi vya luninga kama "friends"Bill Cosby"oprah na wengineo.Je wanaonyesha ule uhalisia wa jamii zao.?Je jamii ndogo kama za wamarekani halisi (wahindi wekundu)wamarekani wa kiasia?Je hawa wamekuwa waki wakilishwa katika hivi vipindi?Nitarejea nikimaliza kuandika kazi yangu ya shule.Hii mada imenikumbusha mengi.