Pages

Monday, October 03, 2005

SAFARI IMEIVA!

Siku,masaa, dakika na hata mwezi sasa unakaribia kuisha tangu ..Sekeseke za mvua za ughaibuni zijulikanazo kama hurricane zipite.Haya mambo yote yalianzia kule Luissiana ambako karibia kila mali iliteketea.,viwanda nyumba,shule ,hospital na sekta zote muhimu.
Basi shughuli na mihangaiko hayakuishia hapo basi sisi majirani wa Luissiana nasi tukapata joto ya jiwe ilikuwa ni kipindi kisicho zidi majuma manne.
Basi hizo hekaheka zikanifika hata mimi mbiu ikapigwa.. kila aliyeko eneo la hatari na hicho kimbembe basi aondeke.Na mimi nikawemo..Nayosema hapa yasikie tu yakikufika utajua.
Basi safari nikaanza siku ya Jumatano mnamo saa tano na nusu nikiwa na lengo la kuelekea Kansas mji wa mbali kutoka hapa nilipo.Muda wa makadirio wa kusafiri ikiwa masaa 6 barabarani.Haya basi hapa ndio nilijuinga na ule uhamaji mkubwa ambao unakaribia kuwekwa kwenye historia ya Marekani.
NITARUDI HIVI PUNDE KUENDELEA NA HIYO HABARI!

No comments: