Pages

Wednesday, July 20, 2005

Je utaanza lini!!

Hili jambo la kujali mazingira na kuheshimu kilichoachwa na kizazi kilichopita kimekuwa ni hadithi...na simulizi sizo isha katika masikio ya wanajamii...
Utunzaji wa mazingira huanzia na wewe mwenyewe kupenda kuvuta hewa safi na kujali kizazi kinachokuja.
Ni hivi karibuni nimekuwa nikisoma makala ya mazingira na kufahamu ubaya zaidi wa hizi hewa chafu ambazo binadamu tuna tengeneza.Tunatengeneza vifaa ambavyo tunatumia kwa muda usiopungua miaka kumi huku vikiachaa maafa ya miaka mia moja ijayo.
Kila siku inapokucha mwanadamu anawaza ni jinsi gani atarahisisha hiki bila kujali ni wa ngapi atakao waathiri.Gesi za magari na mashine nzito nzito ,bandari zinazoshusha mizigo huku zikipuliza gesi zinazochafua anga na kuhatarisha maisha ya viumbe hai,watoto,watu wazima na wazee.
Ni wakati sasa umefika wa kuanza kufikiri na kuweka mtazamo makini kuhusu mazingira.Maana kizazi kijacho kitakuja kutoa hukumu ambayo wewe na mimi tungeiepuka leo hii.
Tunza mazingira,achana na tabia ya kutumia mifuko ya nailoni,chupa za plastiki,kuendesha gari kwa umbali mfupi,tumia usafiri wa umma,acha kutumia madawa kumwagilia bustanini
Kwa wale wanaoweza leo hii amua kutumia gari linalotumia maji tu ama..mafuta ya mimea.Tunza mazingira na yatakutunza..